Blog

Agosti 14, 2018 11:40mu
Mafunzo ya Nenouzima kwa Kiromania
656 Maoni

Mmisheni Bogdan Bilav (mbali kushoto), Mkurugenzi wa Programu ya Lifeword Rick Russell (nyuma yake)
na Bryan Risner (mmishenari mchaguliwa wa Romania, wa tatu kutoka kushoto) akiwa na wanafunzi kumi wa Kiromania
na msaidizi wa Nusfalau, Salaj, Kanisa la Romania.

Kwa miaka minane, Drom de Romangue, matangazo ya dakika thelathini ya Nenouzima, yamekuwa hewani kila Jumamosi usiku huko Ulaya na kwingineko. Bogdan Bilav ni kiongozi wa maono wa Nenouzima (na mjumbe wa BMA) nchini Romania ambaye anaendelea na matangazo na kuwahudumia wasikilizaji wake. Sasa huduma hiyo itapanuka zaidi shukrani kwa mafunzo ya hivi karibuni ya habari yaliyomhusisha Bro. Bogdan, Mkurugenzi wa Programu ya Nenouzima Rick Russell, na kundi la watu wenye shauku kubwa ya kufanya huduma ya habari.

Juma la kwanza la mwezi Desemba, Rick na mimi, pamoja na Mmishenari wa BMA ‘Mati Spencer na Mmishenari Mteule Bryan Risner, tulikwenda Romania ili kushuhudia matangazo ya kihistoria yaliyotengenezwa na wenyeji: Rick alikwenda kuwafundisha, mimi kushuhudia na kurekodi mahubiri tukio ambalo lilitarajiwa kutokea kwa muda mrefu. Siku ya kwanza ya mafunzo, Bogdan na timu yote walikutana na watu hawa kanisani huko Nusfalau, sio mbali na pale anapoishi

Ndugu yetu Bogdan alikuwa ana tafsiri, Rick aliwakaribisha washiriki wa mafunzo kwa maneno yafuatayo: “Kwa mara ya kwanza kabisa, kuna vizazi viwili vya watu, vijana na wazee, ambavyo vimekua kama waumini. Kwangu mimi, ni jambo lisilo la kawaida, na ninafurahi sana kuwa hapa na kuwa sehemu yake.B Bogdan amekuwa akiniambia jinsi jamii ya waumini wa gypsy inavyokua, na sasa tuna uwezo wa kufikia vijiji zaidi.Kwa kuwa wote muna internet mkononi mwenu na unaweza kufikia watu wengi zaidi, wiki hii tunawafundisha namna ya kushiriki imani yako kupitia simu yako. Utakuwa sauti ya watu wa gypsy. ”

Kazi ya kwanza ya Rick kwa washiriki wa mafunzo ilikuwa kutafakari namna gani matangazo yao yanapaswa kuingizwa. Kwanza, aliwaongoza kupitia mjadala wa njia bora ya kufikia watu waliopotea. Mapendekezo yao ya awali kwa yaliyomo yalikuwa ya wazi: kushiriki na kuhubiri Injili, kusoma Biblia, nyimbo na ushuhuda. Hata hivyo, Rick alielezea, walikuwa “wanafikiria kama Wakristo” badala ya kuwa kama siyo Wakristo. Baada ya kuzingatia maslahi yao ya kiutamaduni, ujuzi na ufahamu wao, walielewa, kama mtu mmoja alivyosema, Rick hakuwa “hapa kutuambia kinachofanyika huko Marekani, lakini anatupa nafasi ya kuamua nini kinachoweza kutufanyika kwetu.”

Baada ya majadiliano hayo, Rick alianza mafunzo ya teknolojia kwa kuwapa utaratibu wa namna ya kupakuwa programu ya Spreaker ambayo itatengeneza matangazo yao kutoka “Utangulizi” hadi “kuhitimisha.” Mafunzo ya kila siku yalimalizika na kazi ya “nyumbani” ilitolewa. Siku ya kwanza ya kazi ya nyumbani ilikuwa kutengeneza matangazo ya dakika moja na nusu bila “Utambulisho” na “uhitimishaji.” Programu waliyokuwa wanaitumia kuunda utangazaji inaitwa “Spreaker” na inakuja kamili na namna ya kuchanganya sauti, muziki, na mpaka kumalizia.

Siku ya pili ilianza kwa kusikiliza matangazo hayo waliyokuwa wametengeneza na kuyaelezea. Yalihitimishwa kwa ufafanuzi wa vipengele na zana tofauti katika Spreaker. Kazi yao ya nyumbani kwa siku iliyofuata ilikuwa kuunda matangazo yote kisha kupakua muziki ili uingize ndani yake. Mafunzo ya Siku ya Tatu na Nne yalijumuisha kufanya kazi nje ya ya program ya speaker kwa Wafanyakazi na kutatua matatizo ya kiufundi. Rick pia aliwaagiza kuchapisha matangazo yao “Romanes” (jina la kawaida la lugha yao) ili kuwasaidia wanaotafuta mafundisho kwa njia ya mtandao waweze kupata kwa urahisi. Kazi yao ya siku ya mwisho ilikuwa kukamilisha matangazo yao na kuyaweka kwenye Spreaker na Facebook.

Hatimaye, Siku ya Nne ya mafunzo, walitengeneza mafundisho mubashara ya saa mbili. Watu kumi waaminifu, wadogo na wazee, walikusanyika Jumamosi asubuhi kushiriki mpango ulioandaliwa na kundi la watu wao wenyewe, waliodharauliwa walitoka Ulaya. Watu kadhaa waliposikiliza katika gari la Bogdan na wengine kwenye simu zao za mkononi, wengine walirekodi mahubiri mafupi na nyimbo ambazo walikuwa wakizifanya kila wiki. Msisimko na hisia zao zilionekana na kila mtu katika kanisa hilo ndogo.

Maono ya Bogdan, ambayo amekuwa akiomba kwa miezi mingi, ilikuwa kufundisha na kuhimiza kizazi kipya kutumia “interneti za mikononi” ili kuwafikishia watu wasioamini kila mahali upendo usio na masharti ya Yesu. Mwishoni mwa mafunzo, alimsifu Bwana kwa maombi na mafunzo na msaada wa Nenouzima; lakini Rick, Mati, Bryan na mimi tulikuwa tukishuhudia ndoto hii tukufu ya huduma ya Mungu.

POST COMMENT

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *

Hifadhi
Nembo